123 Nimeketi mimi nili kipofu
1. Nimeketi mimi nili kipofu
Gizani nangojea macho;
Ewe Bwana Yesu mwenye wokovu,
Ondoa dhambi zangu nzito.
Huruma hakuna aonaye,
Gizani nagojea macho,
Sasa nitakase nikusihiye,
Yesu, na dhambi zangu nzito.
2. Tangu siku nyingi nimepofuka
Natamani uso nikwone;
Ewe Bwana Yesu, mwenye baraka
Sema neno, basi, nipone.
3. Nimeketi mimi nili na giza,
Nami ya kutumai sina;
Ili nasikia kunong’oneza,
“Kwake Yesu kuna kupona.”
Comments
Post a Comment