127 Bwana Yesu atakuja
1. Bwana Yesu atakuja, Vumilia!
Omba, ukiwa na haja, Vumilia!
Mbingunu Mungu aliko, Mwamini Mwokozi wako,
Nawe utafika huko, Vumilia!
2. Ikikucheka dunia, Vumilia!
Mwovu atakuvizia, Vumilia!
Hataweza kukushinda, Bwana Yesu akulinda,
Roho yako, akupenda, Vumilia!
3. Na ukiwa hatarini, Vumilia!
Dhiki nyingi duniani, Vumilia!
Vyatupasa kuyakuta, Majaribu na matata,
Na Bwana hakutuficha; Vumilia!
4. Adui wakikutana, Vumilia!
Na ndugu wakikukana, Vumilia!
Zote, zote zitakwisha, Nguvu zote za kutisha
Mungu chini atashusha; Vumilia!
5. Moyoni una majonzi, Vumilia!
Ndiyo bonde-ya-machozi, Vumilia!
Hima tutaandamana, Kwetu Mbinguni na Bwana
Tena hatutaachana; Vumilia!
Comments
Post a Comment