132 Sauti sikilizeni

1. Sauti sikilizeni

Za waimbao juu,
“Aleluya, Aleluya,
Aleluya, mkuu!”
Wako makundi-makundi
Kama nyota wang’ara,
Kwa makuti ya mitende,
Na meupe wamevaa. 
 
2. Wazazi na manabii
Wafanyaji wa njia;
Mashahidi, waandishi,
Nao wafalme pia!
Mabikira kina-mama,
Wajane wa kusali,
Waimba wakikutana
“Msifunu Imanweli”.
 
3. Watu toka huzunini
Wameosha na nguo,
Ni kwa damu yake Yesu;
Maonjo, mbali nao!
Walitekwa, walikatwa
Hata kwa misumeno,
Kwao kifo na shetani
Walishindiwa mno.
 
4. Mungu mumo mwake Mungu,
Nuru mumu mwa nuru,
Kwa kufungamana mwako
Tutaishi mahuru;
Tujalize, Imanweli,
Kujaa kwako wewe
Mungu Baba, Mungu Mwana,
Mungu Roho, tunawe.

Comments

Popular posts from this blog

37 Waitwa, mwovu, na Bwana

52 Yote namtolea Yesu

41 Yesu aliniita