137 Yesu mponya

1. Yesu ndiye mganga wetu

Aponya wagonjwa wote;
Mganga wetu ni Yesu,
Aponyaye hasira. 
 
Tumsifu huyo Yesu
Tumsifu milele,
Kwani Mponya mtakata
Mwokozi wa wanyonge
 
2. Mganga wetu ni Yesu
Huondoa matusi;
Mganga wetu ni Yesu,
Mwenye kuponya choyo.
 
3. Mganga wetu ni Yesu
Huponya wivu wetu;
Yesu ndiye aponyae
Kelele za nyumbani.
 
4. Mganga wetu ni Yesu
Mponya wa tamaa mbaya;
Mganga wetu ni Yesu
Uasherati hufuta
 
5. Mganga wetu ni Yesu
Aponya kiu cha pombe,
Mganga wetu ni Yesu
Kila dhambi uponya

Comments

Popular posts from this blog

37 Waitwa, mwovu, na Bwana

52 Yote namtolea Yesu

41 Yesu aliniita