137 Yesu mponya
1. Yesu ndiye mganga wetu
Aponya wagonjwa wote;
Mganga wetu ni Yesu,
Aponyaye hasira.
Tumsifu huyo Yesu
Tumsifu milele,
Kwani Mponya mtakata
Mwokozi wa wanyonge
2. Mganga wetu ni Yesu
Huondoa matusi;
Mganga wetu ni Yesu,
Mwenye kuponya choyo.
3. Mganga wetu ni Yesu
Huponya wivu wetu;
Yesu ndiye aponyae
Kelele za nyumbani.
4. Mganga wetu ni Yesu
Mponya wa tamaa mbaya;
Mganga wetu ni Yesu
Uasherati hufuta
5. Mganga wetu ni Yesu
Aponya kiu cha pombe,
Mganga wetu ni Yesu
Kila dhambi uponya
Comments
Post a Comment