144 Mbele ninaendelea
1. Mbele ninaendelea,
ninazidi kutembea.
Maombi uyasikie,
Ee Bwana, unipandishe.
Ee, Bwana, uniinue,
Kwa imani nisimame;
Nipande milima yote,
Ee Bwana,
Unipandishe.
2. Sina tamani nikae,
Mahali pa shaka, kamwe;
Hapo wengi wanakaa,
Kuendelea naomba.
3. Nisikae duniani,
asumbuapo Shetani;
Natazamia mbinguni,
nitafika na amani.
4. Nataka nipandishwe juu,
Zaidi yale mawingu.
Nitaomba nifikishwe,
Ee Bwana unipandishe.
Comments
Post a Comment