102 Kazi yangu ikiisha

1. Kazi yangu ikiisha, nami nikiokoka;

Na kuvaa kutokuharibika,
Nitamjua Mwokozi nifikapo ng’amboni;
Atakuwa wa kwanza kunilaki.
 
Nitamjua, nitamjua, nikimwona uso kwa uso;
Nitamjua, nitamjua, kwa alama za misumari. 
 
2. Furaha nitapata nikiona makao
Bwana aliyotuandalia;
Nitamsifu mwokozi kwa rehema na pendo
Vilivyonipa pahali Mbinguni.
 
3. Nao waliokufa katika Bwana Yesu,
Nitawaona tena huko juu;
Lakini nifikapo kwake huko Mbinguni,
Nataka kumwona Mwokozi kwanza.
 
4. Milangoni mwa mji Bwana atanipitisha,
Pasipo machozi wala huzuni.
Nitauimba wimbo wa milele; lakini
Nataka kumwona Mwokozi kwanza. 

Comments

Popular posts from this blog

37 Waitwa, mwovu, na Bwana

52 Yote namtolea Yesu

41 Yesu aliniita