111 Neno lako Bwana
1. Neno lako, Bwana,
Ni imara sana;
Lilo latwongoza,
Lilo latufunza.
2. Adui wabaya
Wakikaribia,
Neno lake Bwana
Ni ulinzi sana.
3. Siku za dhoruba
Soma ukiomba;
Neno lake Bwana
Msaada sana.
4. Ukiliamini,
Hwenda na amani;
Una na furaha
Neno ni siraha.
5. Ni furaha kweli,
Na wingi wa mali,
Neno lake Bwana
Kwa wasiokana
6. Neno la rehema,
Tukali wazima;
Faraja I papo,
Tufarikanapo.
7. Tulijue sana
Neno lako, Bwana,
Hapa tukupende,
Kisha kwako twende.
Comments
Post a Comment