111 Neno lako Bwana

1. Neno lako, Bwana,

Ni imara sana;
Lilo latwongoza,
Lilo latufunza.
 
2. Adui wabaya
Wakikaribia,
Neno lake Bwana
Ni ulinzi sana.
 
3. Siku za dhoruba
Soma ukiomba;
Neno lake Bwana
Msaada sana.
 
4. Ukiliamini,
Hwenda na amani;
Una na furaha
Neno ni siraha.
 
5. Ni furaha kweli,
Na wingi wa mali,
Neno lake Bwana
Kwa wasiokana
 
6. Neno la rehema,
Tukali wazima;
Faraja I papo,
Tufarikanapo.
 
7. Tulijue sana
Neno lako, Bwana,
Hapa tukupende,
Kisha kwako twende.

Comments

Popular posts from this blog

37 Waitwa, mwovu, na Bwana

52 Yote namtolea Yesu

41 Yesu aliniita