116 Bwana , U sehemu yangu

1. Bwana u sehemu yangu,

Rafiki yangu wewe;
Katika safari yangu
Tatembea na wewe;
Pamoja na wewe,
Pamoja na wewe,
Katika safari yangu
Tatembea na wewe. 
 
2. Mali hapa sikutaka,
Ili niheshimiwe,
Na yanikute mashaka
Sawa sawa na wewe,
Pamoja na wewe,
Pamoja na wewe,
Heri nikute mashaka
Sawasawa na wewe.
 
3. Niongoze safarini,
Mbele unichukue
Mlangoni kwa Mbinguni
Niingie na wewe.
Pamoja na wewe,
Pamoja na wewe,
Mlangoni kwa mbinguni,
Niingie na wewe.

Comments

Popular posts from this blog

37 Waitwa, mwovu, na Bwana

52 Yote namtolea Yesu

41 Yesu aliniita