117 Tufani inapovuma
1. Tufani inapovuma
Sana moyoni mwangu,
Huona pa kujificha
Mkononi mwa Mungu.
Hunificha, hunificha
Adui hatanipata,
Hunificha, hunificha,
Mkononi mwake.
2. Pengine kuna taabu
Yanisongeza kwake;
Naijua si hasira,
Ni ya mapenzi yake.
3. Adui wakiniudhi
Nami nikisumbuka,
Mungu atavigeuza
Vyote viwe baraka.
4. Niishipo duniani
Ni tufani daima,
Anilindapo rohoni
Nitakaa salama.
Comments
Post a Comment