99 Maelfu na maelfu

1. Maelfu na maelfu

Wenye nguo bora!
Masafu ya waongofu
Wenye na bendera!
Amekwisha kamili
Vita vya shetani
Fungueni lango hili;
Njoni, ingieni! 
 
2. Imbeni aleluya,
Zipae Mbinguni!
Pigeni sana sauti
Kwa kutumaini!
Kwa hiyo viliumbwa
Nchi hata Mbingu
Dhiki za muda zikisha,
Asifiwe Yesu.
 
3. Loo! Tukionana
Pwani ya ng’amboni!
Loo! Tukishirikiana
Milele Mbinguni!
Midomo yote pia,
Huko itaimba
Wajane kufufukiwa
Na kila yatima!
 
4. Himiza enzi yako,
Uliyetufia
Utimize watu wako,
Wakosaji pia,
Mpendwa wa taifa
twakutumaini!
Uzifunue ishara
Urudi enzini! 

Comments

Popular posts from this blog

37 Waitwa, mwovu, na Bwana

52 Yote namtolea Yesu

41 Yesu aliniita