40 Nasikia kuitwa

1.  Nasikia kuitwa

Na sauti yako
Nikasafiwe kwa damu
Ya kwangikwa kwako.

Chorus:
Nimesogea Mtini pako,
Unisafi kwa damu ya kwangikwa kwako.
 
2.  Ni mnyonge kweli,
Umenipa nguvu,
Ulivyonisafi taka,
Ni utimilivu.
 
3.  Yesu hunijuvya;
Mapenzi imani,
Tumai, amani, radhi,
Hapa na Mbinguni.
 
4.  Huipa imara,
Kazi yake, ndani:
Huongezeka neema,
Ashindwe Shetani.
 
5.  Huishuhudia,
Mioyo ya imani
Ya kuzipata ahadi,
Wakimuamini.
 
6.  Napata wokovu,
Wema na neema;
Kwako Bwana nina nguvu
Na haki daima.

Comments

Popular posts from this blog

37 Waitwa, mwovu, na Bwana

52 Yote namtolea Yesu

41 Yesu aliniita