46 Twae wangu uzima
1. Twae wangu uzima,
Sadaka ya daima;Twae saa na siku
Zikutukuze huku.
2. Twae mikono nayo,
Ifanye upendavyo,
Twae yangu miguu
Kwa wongozi wako tu.
3. Twae sauti yangu,
Niimbe kwa Mungu tu;
Itwae na midomo,
Ijae neno lako.
4. Twae dhambi pia,
Na yote ya dunia;
Twae yangu hekima,
Upendavyo tumia.
5. Njia itwae, Mungu,
Haitakuwa yangu;
Twae moyo; ni wako,
Uwe makazi yako.
6. Twae mapenzi yangu,
Sifa za moyo wangu;
Twae kabisa nafsi
Nniwe wako halisi.
Comments
Post a Comment