49 Nitwae hivi nilivyo
1. Nitwae hivi nilivyo,
Umemwaga damu yako,Nawe ulivyoniita,
Bwana Yesu, naja, naja.
2. Hivi nilivyo; si langu
Kujiosha roho yangu;
Nisamehe dhambi zangu,
Bwana Yesu, naja, naja.
3. Hivi nilivyo; sioni
Kamwe furaha moyoni;
Daima ni mashakani,
Bwana Yesu, naja, naja.
4. Hivi nilivyo kipofu,
Maskini na mpungufu;
Wewe u mtimilifu;
Bwana Yesu, naja, naja.
5. Nawe hivi utanitwaa;
Nisithubutu kukawa,
Na wewe hutanikataa,
Bwana Yesu, naja, naja.
6. Hivi nilivyo; mapenzi
Yamenipa njia wazi;
Hali na mali sisazi,
Bwana Yesu, naja, naja.
Comments
Post a Comment