55 Nipe moyo wenye sifa
1. Nipe moyo wenye sifa
Sio wa utumwa;Moyo ulionyunyizwa
Damu ya thamani.
2. Moyo maskini, moyo
Wa kunyenyekea,
Moyo utawaliwao
Na Mwokozi pia.
3. Mwenye kutubu, mnyonge,
Sadiki, amini;
Kamwe, kamwe asitengwe
Akaaye ndani.
4. Mpya, mwema na mawazo
Mwingi wa mapenzi
Nawe uwe kielelezo
Moyo wa Mwokozi.
5. Ni uule moyo wako;
Moyo wa huruma
Yesu, natamani kwako
Kukujua vyema.
6. Na ya midomo matunda
Yako, nipe nami;
Amani isiyokoma
Iwe yangu mimi.
7. Nitie yako tabia,
Inishukie juu;
Jina lako nipe pia,
Ndilo la pendo tu.
8. Ni wa Baba utukufu;
Mwana atukuke;
Na roho Mtakatifu
U Utatu pweke.
Comments
Post a Comment