40 Nasikia kuitwa
1. Nasikia kuitwa Na sauti yako Nikasafiwe kwa damu Ya kwangikwa kwako. Chorus: Nimesogea Mtini pako, Unisafi kwa damu ya kwangikwa kwako. 2. Ni mnyonge kweli, Umenipa nguvu, Ulivyonisafi taka, Ni utimilivu. 3. Yesu hunijuvya; Mapenzi imani, Tumai, amani, radhi, Hapa na Mbinguni. 4. Huipa imara, Kazi yake, ndani: Huongezeka neema, Ashindwe Shetani. 5. Huishuhudia, Mioyo ya imani Ya kuzipata ahadi, Wakimuamini. 6. Napata wokovu, Wema na neema; Kwako Bwana nina nguvu Na haki daima.